Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Chuo cha Taifa cha Ulinzi - Tanzania

Colonel Kosgey Kimeli
Mshiriki wa Kozi ya Kumi na moja kutoka Kenya
Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania (NDC-TZ) ni Taasisi inayoongoza kwa kuimarisha kipengele muhimu zaidi cha usalama wa Taifa. Chuo hiki kimekuwa ni kiungo muhimu katika kuhakikisha kwamba viongozi, watendaji wa usalama na wataalam wanakuwa bora ili kuendana na mienendo ya kimkakati kwa mazingira ya usalama na yanayobadilika kila mara.
Ms. Neema Mwakalyelye, ndc
Naibu Mkurugenzi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)
‘Nikiri wazi kwamba wiki 47 nilizokaa NDC zimenipandisha kwenye kiwango cha juu cha ujuzi na uelewa wa wajibu wangu kama raia, mtumishi wa umma na kiongozi katika masuala ya usalama wa Taifa. Kozi imenifundisha kufikiri na kufanya mabo kwa njia tofauti. Kusema kweli nimejitolea zaidi kuona kwamba mikakati ya Serikali inalenga kuifanya Tanzaniakuwa mahali salama, sio tu kutokuwa na migogoroya ndani na vita bali pia kwa Tanzania kuwa sehemu ambayo fursa za ajira ni kubwa, watu wana afya njema, utawala bora unatekelezwa na amani ipo.’